Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Uchizi wa Facebook na Instagram huu hapa!

Facebook  na Instagram  zimewatia watu uchizi.
  1. Mtu anaamka kichwa kinamuuma kishenzi, anamtuma mtu dukani akanunue vocha ya alfu, kisha ananunua bando ili apost kwenye FB na Insta …kichwa kinaniua.. si ile hela ungenunua panadol upone kichwa?
  2. Mwanae homa imepanda, anamtuma hauzgelo akanunue vocha, badala ya kumpigia simu mumewe wampeleke mtoto hospitali, ananunua bando halafu anapost FB, ‘Mungu akuponye mapema mwanangu’
  3. Kapata lift kwenye gari anajipiga selfie anatuma instagram, ‘Driving to work’
  4. Kwa mara ya kwanza baada ya miezi kaingia kanisani, padri aliposema tufunge macho tuombe, anapost eti ‘Feeling Blessed’

Post a Comment

0 Comments