
Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na waandishi
wa gazeti hili, nyumbani kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Na
Mpiga Picha Wetu.
---
Hofu kuhusu nafasi ya CCM kwenye Uchaguzi Mkuu ujao inazidi
kuongezeka baada ya mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki
kukitabiria chama hicho tawala “kazi kubwa”, akisema hali ya sasa “siyo
ile iliyokuwa nayo miaka mitano iliyopita”.
Kagasheki pia alikitahadharisha chama hicho dhidi
ya kuzidi kukua kwa nguvu ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) akisema
iwapo umoja huo utamchagua mgombea makini, CCM itakuwa na kazi ngumu.
Balozi Kagasheki, ambaye alikuwa Waziri wa
Maliasili na Utalii kabla ya kujiuzulu kutokana na sakata la Operesheni
Tokomeza, alisema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa mahojiano maalum na
gazeti la Mwananchi.
Kauli yake inaungana na za vigogo wengine wa CCM
waliotahadharisha mwenendo wa chama hicho dhidi ya ongezeko la nguvu ya
upinzani, akiwamo Waziri Mkuu wa zamani, Fredrick Sumaye, ambaye alisema
rushwa inakimaliza chama hicho, na Naibu Waziri wa Sayansi na
Teknolojia, January Makamba, ambaye alisema kuwa chama hicho kisitegemee
ushindi wa kishindo.
0 Comments
Unapenda kuhabarika? Jiunge nasi Katika Twitter na Facebook ili tuhabarishane.
Kumbuka Kuacha maoni yako hapa pindi usomapo habari zetu. Karibu Tena