Header Ads Widget

Responsive Advertisement

News Alert:FFU watumia mabomu ya Machozi kuwatawanaya wafuasi wa CUF Temeke huku Prof Lipumba akikamatwa

Habari zilizotufikia katika Mtandao wa Rorya Finest Blog kutoka kwa mmoja wa wadau waishio Wilaya ya Temeke Jijini Dar, zinasema kuwa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam limetumia mabomu ya Machozi ili kuwatawanya Wafuasi na wapenzi wa Chama cha Wananchi CUF waliokuwa wakiandamana kuelekea Mbagala kwaajili ya kuwakumbuka wanachama wenzao waliopoteza maisha Huko Zanzibar Januari 26,2001.

Jeshi hilo limefanikiwa kuwatia nguvuni viongozi waandamizi wa chama hiko wakiongozwa na Mwenyekiti wao Taifa Prof Ibrahim Lipumba.

Akithibitisha kukamatwa kwa viongozi hao pamoja na Mwenyikiti wao Afisa Habari wa CUF, Bw Silas amekaririwa akisema Kuwa walianza maandamano ya amani katika viwanja vya Temeke na Kuelekea Mbagala ambapo maandamano hayo yaliyokuwa na lengo la kuwakumbuka wanachama wa CUF waliopoteza maisha Januari 26 2001 katika maandamoo huko Zanzibar na Tanzania Bara.

Bw Silas aliongezea kuwa wakati walipofika Mtoni Mtongani, Wilaya ya Ilala Manispaa ya Temeke Jeshi la Polisi liliwasili na kuanza kurusha mabomu ya machozi na Kuwapiga Wanachama na hatimaye kufanikiwa kuwatia nguvuni viongozi waandamizi wa chama hiko na kuwapeleka kituo kikuu cha Polisi. Sababu za kuwakamata wanachama wa CUF na viongozi wao huku sababu za kukamatwa kwao zikielezwa kuwa ni kufanya maandamano bila kuwa na kibali.

Post a Comment

0 Comments