Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Kingine ambacho huenda hujasikia kuhusu ishu ya ajali ya ndege ya TransAsia…

taiwan-plane-crash0bd21-6
Baadhi ya ndugu wakilia wakati wa kupokea miili ya ndugu zao waliofariki kwenye ajali hiyo.
Familia za ndugu wa watu waliopata ajali kwenye ndege ya TransAsia Airlines GE235 ambayo ilianguka muda mfupi baada ya kuruka kutoka uwanja wa ndege Taipei, wamekutana na uongozi wa Kampuni hiyo jana na kujadili mambo kadhaa ikiwemo malipo ya fidia na rambirambi za marehemu waliofariki katika ajali hiyo.
Liu Zhongji ni mwakilishi wa Kampuni hiyo ya ndege Taiwan, ametoa maelezo kuhusu kilichozungumzwa katika kikao kilichokaa zaidi ya saa tatu ambapo wanafamilia hao wamekataa kulipwa jumla ya dola milioni 14.9 za Taiwan (zaidi ya Ths. Milioni 850/-) ambayo wangepatiwa ndugu hao kwa kila mtu mmoja aliyefariki kwenye ajali hiyo.
Kiasi hicho cha pesa kilipangwa kutolewa kwa ajili ya kusaidia shughuli za mazishi pamoja na rambirambi kwa wafiwa hao.
taiwan-plane-ap-780
Vikosi vya ukoaji wakivuta mabaki ya ndege kutoka kwenye mto ilikoanguka.
Ajali hiyo ilisababisha kifo cha watu 42, wengine 15 walifanikiwa kutoka salama huku mwili wa mtu mmoja ukiwa bado unatafutwa, ajali hiyo ilitokea muda mfupi baada ya engine ya ndege hiyo kupata hitilafu na kuifanya ndege hiyo kupoteza mwelekeo, ikagonga ukingo wa daraja na kuanguka mtoni.
Janga lingine limewakuta marubani wa Kampuni hiyo ambapo baada ya ajali hiyo kutokea walilazimika kuwapa mtihani uliofanya 29 kati yao kusimamishwa kazi baada ya kufanya mtihani huo uliowapima namna wanavyoweza kupambana na kuokoa ndege iliyopata dharura.
Taiwan-Plane-Crash
Picha iliyopigwa na camera ya kwenye gari wakati ndege hiyo ikianguka.
Hii ni taarifa ambayo iliripotiwa kuhusu ajali hiyo FEBRUARY 4 na kituo cha CNN

Post a Comment

0 Comments