Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Michezo | YANGA yaifumua Ndanda FC 4-0 yaikaribia Simba..

Image result for Yanga na Simba
Yanga imeendelea kuipa presha na kuipumulia Simba inayoongoza ligi kuu Tanzania bara kwa pointi 41 baada ya kuifumua Ndanda kwa bao 4-0 katika mchezo mkali liofanyika kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam

Mlinzi wa Yanga Vicent Bossou alihitimisha kalamu ya ushindi kwa kufunga bao la nne katika dakika ya 89 kwa kichwa akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na mlinzi mwenzake, Juma Abdul.

Amis Tambwe alipachika bao la tatu dakika ya 26 huku Donald Ngoma akifunga mabao mawili katika dakika ya 21 na dakika ya tatu kwenye mchezo huo akiwa na magoli 37 katika klabu msimu huu kutokana na ushindi huo Yanga imefikisha pointi 40 dhidi ya Simba yenye pointi 41. 

Kikosi cha Yanga dhidi ya Ndanda ni:-
1.Deogratius Munishi
2.Juma Abdul 
3.Mwinyi Haji
4.Vicent Bossou
5.Kelvin Yondani
6.Saidi Juma
7.Saimoni Msuva
8.Haruna Niyonzima
9. Donald Ngoma
10. Amisi Tambwe
11.Emanuel Martin

Akiba 
Ali Mustafa
Andrew Vicent
Justin Zullu
Thabani Kamusoko
Obrey Chirwa
Geofrey Mwashuiya
Deusi Kaseke.

Post a Comment

0 Comments