Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Kimataifa | Boko Haram Imewateka Nyara Watafiti wa Mafuta Nigeria

Image result for Boko Haram
Kampuni ya mafuta ya Nigeria N-N-P-C, inasema kuwa watafiti 10 wa jiologia, wametekwa nyara na washukiwa wa kundi la Boko Haram
Wanajiolojia hao na masoroveya wa Chuo Kikuu cha Maiduguri, waliviziwa na kutekwa nyara karibu na kijiji cha Jibi kilichoko katika jimbo la Borno, Kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Walikuwa wamepewa kandarasi ya kutafuta mafuta karibu na ziwa Chad.
Taarifa nyingine kutoka maeneo hayo, inasema kuwa kuna hofu wameuawa, lakini hilo halijathibitishwa.
Hatahivyo habari za hivi karibuni zimebaini kuwa mmoja ya watafi hao amepatikana.
Msemaji wa NNPC Ndu Ughamadu alithibitisha kwa BBc kwamba Ibrahim Gildado alipatikana akiwa hai lakini hakutoa maelezo zaidi.
Baadhi ya maafisa wa usalama waliokuwa vijana wa kuweka amani mtaani wanaotoka katika eneo hilo pia walipatikana

Post a Comment

0 Comments