Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Soma alichokiandika >>> "MAFANIKIO Ya Diamond platnumz Yananinyim Amani". Asema Linex..


Kuna uwezekano Linex Sunday Mjeda akawa ni msanii ambaye kwa kile alichokisema akawa anawakilisha mawazo ya wasanii wengi, kutokana na hatua kubwa anazoendelea kuzipiga msanii mwenzao Nasib Abdul aka Diamond.

Ukiachana na mengi ambayo tayari ameyafanya kama msanii na kama Mtanzania anayepeperusha bendera ya nchi yake huko duniani, Platnumz amekuwa chachu ya maendeleo kwa wasanii wenzake ambao kwa namna moja au nyingine wanatamani kufikia mafanikio yake.

Linex ameguswa na hatua aliyofikia Platnumz ambaye bado yuko Marekani alikoenda kuhudhuria tuzo za BET, na kuamua kueleza kile kilicho moyoni. Amepost picha ya Platnumz akiwa na msanii wa Marekani Nelly, na kuandika ujumbe huu.
“Kutoka moyoni this step ya uyu mwana ina ninyima usingizi but haininyimi kwa ubaya inaninyima kwa uzuri na inanipa msukumo wa kupiga kazi na kuamin Mungu aliweka kitu ndani yangu kwa maksud big S/o @diamondplatnumz nachoamn mm ni umefungua njia za mziki wa tanzania#wemakwaubaya #Wethevoa.”

Huu ni wakati kwa wasanii kuwaunga mkono wale wanaostahili na kuiga mifano yao ili kuikuza sanaa ya Tanzania hasa kimataifa.

Post a Comment

0 Comments