Header Ads Widget

Responsive Advertisement

News | Mnyika, Maghufuli na Mdee walipokutana katika shughuli za Maendeleo

Waziri wa Ujenzi Dr Joh Magufuli, Mbunge wa Jimbo la Ubungo-Chadema  John Mnyika,Mbunge wa Jimbo la Kawe -Chadema Halima Mdee,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadic Wakizindua  ujenzi wa barabara wa barabara ya External –Kilungule
 Waziri wa Ujenzi Dr Joh Magufuli, Mbunge wa Jimbo la Ubungo-Chadema  John Mnyika,Mbunge wa Jimbo la Kawe -Chadema Halima Mdee,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadic Wakizindua  ujenzi wa barabara ya Msewe-Baruti
  Waziri wa Ujenzi Dr Joh Magufuli, Mbunge wa Jimbo la Ubungo-Chadema  John Mnyika,Mbunge wa Jimbo la Kawe -Chadema Halima Mdee,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadic Wakizindua  ujenzi wa barabara ya Mbezi mwisho-Goba-Tangi Bovu
 Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika, Waziri wa Ujenzi, Dkt John Magufuli na Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee mara baada ya kuzindua mitambo itakayofanya kazi katika ujenzi wa barabara ya Mbezi mwisho-Goba-Tangi bovu
 Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika, Waziri wa Ujenzi, Dkt John Magufuli na Mbunge wa Jimbo la Kawe, wakisalimiana na wananchi baada ya kuzindua mitambo itakayofanya kazi katika ujenzi wa barabara
  Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika akizungumza na Waziri wa Ujenzi, Dkt. Pombe Magufuli

Muonekano wa sasa katika hatua za awali za ujenzi wa barabara ya Mbezi mwisho-Goba-Tangibovu eneo la Goba
---
 
Babaraba zilizowekewa mawe ya msingi ni pamoja na ile ya Kinyerezi-Kifuru hadi Mbezi Mwisho yenye urefu wa kilometa 14.0, Kigogo-Tabata Dampo yenye urefu wa kilometa 1.6 na Kimara Baruti-Msewe hadi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yenye urefu wa kilomita 2.6

Barabara nyingine ni ile ya External-Kilungure hadi Kimara Korogwe kilometa 8.0, Wazo Hill-Goba hadi Mbezi Mwisho kilometa 20 na Goba-Tangi bovu kilometa 9.0

Waziri Magufuli  alisema, barabara ya Wazo Hill-Goba yenye urefu wa kilometa 20 ikikamilika kwa kiwango cha lami itaziunganisha barabara za  Bagamoyo na Morogoro ambazo zimekuwa zikikabiliwa na msongamano kwa muda mrefu.

Pia, barabara ya Kinyerezi-Kifuru hadi Mbezi Mwisho yenye urefu wa kilometa 14 itapunguza msongamano kwa kiasi kikubwa kwa kuwa itakuwa inaunganisha barabara ya Morogoro na Nyerere.

Kwa umuhimu sana, Waziri Magufuli alisisitiza; "kumbukeni mkiiba vifaa vya ujenzi hamuibi vifaa vya kampuni zinazojenga bali mnajiibia wenyewe kwa sababu hizi ni fedha za kodi ya wananchi bali kwa kufanya kazi kwa bidii na uadilifu kutawezesha ujenzi wa barabara kukamilika kwa wakati na ninyi (mafundi) kujihakikishia uhakika wa ajira"

Naye Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng.Patrick Mfugale ameiomba serikali kuongeza bajeti ya barabara ili kuwezesha miradi ya barabara kukamilika kwa wakati na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa wakandarasi ili barabara zijengwe kwa kiwango kilichokubalika katika mikataba.

Post a Comment

0 Comments