Header Ads Widget

Responsive Advertisement

KUMEKUCHA TARIME | 11 WAJITOKEZA KUCHUKUA FORM ZA UBUNGE KWA TIKETI YA CHADEMA

Picha ya mwenyekiti wa chadema wilaya ya Tarime Lukas Ngoto akirudisha fomu jana  ya kuwania jimbo la Tarime Mjini ni katika ofisi ya chadema Wilaya.
Wanao wania ubunge Tarime mjini na vijijini wafika 11 chadema.
Katika mchakakato uliopo wa kuwania uongozi kupitia ngazi mbalimbali ukiwemo Ubunge  Udiwani na Urais Wilayani Tarime Mkoani Mara mpaka sasa walijitokeza kuwania ubunge baada ya jimbo kugawanya wamefikia 11.

Aidha watia nia hao kwa upande wa Ubunge Jimbo la Tarime Mjini waliotanagaza nia ni Watano ambao ni Lukas Ngoto  Mwenyekiti wa chama Wilaya   Esther Matiko Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Mara  Chadema , Charles Werema , Maritinus Joseph na Christopher Chomete. Huku jimbo la Tarime Vijijini akiwa ni Jonh Heche aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Taifa ,  Piter Bhusene, Moses Yomami Mwenyekiti wa Baraza la Vija Wilaya ambaye pia ni Mwanasheria kaanda ya Serengeti , Joanes Manko, Fabian Mwita na Prosper Nyamuhanga huku jumla wakiwa kumi namoja,

Akirudisha fomu ya kuwania ubunge jimbo la Tarime Mjini Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Lukas Ngoto amesema kuwa ameamua kuwania kiti hicho kwa lego la kuwawakilisha wananchi wote.

Kupitia Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Wilayani Tarime  Mkoani Mara Thobias Elias Ghati  chama hicho kimesema kuwa kikotayari kushirikiana na wagombea wote waliotangaza kuwania jimbo la Tarime Mjini na Vijiji kwa lengo la kupata kiongzi bora ambao watawatumikia wananchi kwa lengo la kuleta Maendeleo ndani ya Wilaya ya Tarime Mjini na Tarime Vijijini huku katibu huyo akitaja mnamo 23 julai mwaka katika ukumbi wa chuo cha ualimu kutafanyika upigaji wa kura z maoni ili kupata viongzi wawili watakao peperusha bendera ya chama hicho upande wa jimbo la Tarime Mjini na Vijijini,

Sanjari na hayo kwa leo Mbunge wa viti maalumu kupitia chadema Mkoa wa Mara Esther Matiko anategemea kupokelewa na watanzania huku akirejea majimboni kwa lengo la kuongea na watanzania na badae atakuwa na mkutano wa hadhara katika viwanja vya soko la rebu wilayani hapa. Kwa lengo la kuongea na wananchi kuhusu msitakabari wake na vipaumbele  kwani naye ni mmoja kati ya wanaowania jimbo la Tarime Mjini na ni mwanamke pekee aliyedhubutu kati ya waliojitokeza 11

Post a Comment

0 Comments