Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Rorya | RC Mara afanya ziara ya kushtukiza kuona maendeleo ya wanufaika wa Mradi wa TASAF wilayani Rorya

Image may contain: 5 people, people standing and people sitting
Mkuu wa Mkoa wa Mara Dr Charles Mlingwa ametembelea zaidi ya kaya 30 ambazo zinanufaika na mradi wa TASAF kuwasikiliza walengwa na kuona changamoto na mafanikiyo waliyo yapata kutokana na mradi.
Image may contain: 2 people, outdoor and nature
Akiwa kijijini Utegi amemtembelea ndgu Okeyo Ogola na kumkuta pesa anazopata ameanza kuchimba shimo la choo na bafu na ambapo mkuu wa wilaya Saimoni Kimori Chacha alimsaidia sementi 5 na kaimu mkurugenzi wa Rorya ndugu Mhando kumchangia mabati matano5.ili akamilishe ujenzi wa choo na bafu.
NYANDUGA:
Ndugu Joseph Matara wa kijiji cha Nyanduga ameondolewa kwenye mpango wa TASAF baada ya kuonekana uwezo wa kufanya kazi anao na fursa za kiuchumi anazo ikiwepo miti ya natunda kama vile maparachichi,maembe na shamba lenye rutuba.lakini hata pesa anazo pokea hakuonyeaha mpango hata wakununua walau kuku.ili kuweza kusimama baada ya mradi kumalizika.
Image may contain: one or more people, people standing, grass, plant, tree, outdoor and nature
RIAGORO:
Samweli Atoo Matinde ambae ni mlemavu ni fundi baiskeli ameweza kunufaika na mradi baada ya pesa anazopata ameweza kununua mbuzi ,kuku na kununua mabati na kufanikiwa kujenga nyumba ya vyumba vitatu kwa kuwa na mpango wa kujikwamua kutoka katika hali ya nyuma aliyokuwa nayo. ambapo kwa kuonyesha jitihada hizo Mkuu wa mkoa Dr Charles mlingwa amempa mifuko 5 ya sementi kwa ajili ya kukamilishia choo na bafu.ndugu Samweli amemshukuru mkuu wa mkoa kwa kumuwezesha atamalizia choo na bafu lake.
Image may contain: 5 people, people standing
INGRIJU:
Simion Choda ambae ni kipofu alipo tembelewa na timu iliyo ongozana na mkuu wa mkoa walimpongeza kwa kutumia vizuri pesa kidogo anayo pata ikiwa ni kusomeshea wajukuu zake na kufanikiwa kujenga choo na bafu.ambapo mkuu wa mkoa Dr Charles alimpatia mifuko 5 ya sementi kwa ajili ya kumalizia choo na bafu.
Kwa kuhitimisha ziara yake wilayani Rorya mkuu wa mkoa kwa Mara Dr Charles mlingwa amesema nilazima viongozi wachukue hatua za maksudi kuhakikisha kila kaya ina choo na bafu cha kisasa ili kupungiza magonjwa ya mlipuko.amesema kinacho leta kipindu pindu ni kinyesi kama watu wanakosa vyoo ma kujisaidia vichakani na inaponyesha mvua maambukizi yanakuwa yanaenea kwa njia ya maji machafu .
Alipokuwa njiani kurudi Musoma mkuu wa mkoa alikuta mkutano wa hadhara ulioitishwa na mh Nyawambo diwani wa kata ya Mirare kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kuchangia ukenzi wa madarasa ya shule ya sekondari ya mirare baada ya kuepo na upungifu wa madarasa na kusababisha wanafunzi walio chaguli mwaka Jana kukosa vyumba vya kusomea ,ambapo mkuu wakoa Dr mlingwa aliguswa na kuchangia mifuko 25 ya sementi kuwaunga mkono wanainchi wa mirare kwa juhudi ya kuunga tamko la Mh. Dr John Pombe Magufuli kwa elimu bure kwa kila mtoto anaezaliwa Tanzania.

Post a Comment

0 Comments