Header Ads Widget

Responsive Advertisement

KISUMWA | Mvua yaleta maafa shule ya Sekondari Kisumwa

Image may contain: one or more people, cloud, sky, mountain, nature and outdoorImage may contain: cloud, sky, house, outdoor and nature
MVUA kubwa zilizoambatana na upepo mkali zimeleta maafa makubwa katika shule ya SEKONDARI KISUMWA.
Mvua kubwa na upepo mkali ulio chukua takribani saa moja na robo imeleta madhara makubwa
Nyumba 2 za maabara zimeanguka /zimebomoka na kuanguka chini, jengo moja la maabara limeezuliwa,madarasa matatu yameezuliwa, Vyoo vya wanafunzi na waalimu vimebomoka.
Image may contain: sky, cloud, house, outdoor and nature
Akizungumza na kituo cha habari Ofisini kwake, Mkuu wa wilaya ya Rorya Mhe. Saimoni Kimori Chacha amesema uharibifu ulio tokea ni mkubwa sana na amesema mkurugenzi wa halimashauri wamechukua hatua za dharura kuhakikisha wanarudisha haraka miundombinu ili wanafunzi waendelee na masomo.
Image may contain: outdoor and nature
Mkuu wa wilaya amewataka viongozi wanaosimamia ujenzi kusimamia kwa umakini kwani inaonyesha majengo mawili ya maabara hayakujengwa kwa kiwango cha kutosha kulingana na jinsi yalivyobomoka tofauti ya darasa ambalo liliezuliwa na ukuta kuonekana imara lakini Yale majengo ya maabara kiwango chake hakikukidhi viwango vya ubora.
Image may contain: tree, plant, outdoor and nature
Ametaka pesa za wananchi zinazoelekezwa kwenye miradi ya wananchi kuwepo na nidhamu ya usimamizi wa pesa hizo na kufanya kazi katika kiwango kinachotakiwa 

Image may contain: 1 person, sitting and indoor
Picha na kituo cha habari na mawasiliano utegi Rorya

Post a Comment

0 Comments