Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Hivi Ndivyo Magufuli Alivyozindua Barabara ya Igawa-Rujewa

 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiweka jiwe la msingi kuashiria ufunguzi wa barabara ya Igawa-Rujewa KM 9.8 iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro pamoja na viongozi wengine wa Wilaya ya Mbarali.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akikata utepe kuashiria ufunguzi wa barabara hiyo. Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro pamoja na viongozi wengine.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa barabara nchini TANROADS Eng. Patrick Mfugale akisoma taarifa ya mradi wa barabara ya Igawa-Ubaruku inayojengwa kwa kiwango cha lami.
 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akiwahutubia wakazi wa Ubaruku na Rujewa Wilayani Mbarali.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwahutubia wakazi wa Rujewa na Ubaruku wilayani Mbarali kuhusu ujenzi wa barabara ya Igawa-Ubaruku km 18.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akifurahia ngoma pamoja na kikundi cha ngoma za asili cha Rujewa mara baada ya kuwahutubia wakazi wa Rujewa na Ubaruku wilayani Mbarali.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiagana na wakazi wa Rujewa na Ubaruku mara baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara.

Post a Comment

0 Comments