Header Ads Widget

Responsive Advertisement

AFYA YAKO | BAMIA NA FAIDA ZAKE KATIKA KUTIBU MAGONJWA MBALIMBALI MWILINI

Bamia ni mboga ambayo inafahamika na watu wengi na imekuwa ikitumiwa na watu wengi hapa nchini Tanzania.

Pamoja na bamia kuwa mboga, lakini pia inafaida nyingi katika miili yetu, licha ya kuwa wengi wetu huwa hatufahamu faida zake zaidi ya kula tu kama mboga.
Miongoni mwa faida za mboga hii ni pamoja na kusaidia kuondosha vimelea vya sumu kwenye ngozi, inasaidia pia kuimarisha afya ya nywele na kuongeza kinga ya mwili.
  
Pia bamia husaidia kuondoa uchovu wa mwili na msongo wa mawazo pamoja na kusaidia kutibu tatizo la kukosa choo.
Aidha, bamia pia inaelezwa kusaidia kusafisha damu, kutibu mafua, vidonda vya tumbo, inaimarisha mifupa pamoja na kuwa kinga ya magonjwa kama utapiamlo na anemia.
Mbali na hayo bamia pia inasaidia kutibu  magonjwa  mbalimbali  ya  zinaa  kama vile  kaswende na kisonono. Vilevile  inaponya  tatizo  la  kwenda  hedhi  mara  kwa  mara na  chango la kike.
Hizo ni baadhi ya faida za ulaji wa bamia, endapo utaendelea kutembelea tovuti hii mara kwa mara basi utazidi kupata elimu zaidi juu ya namna vyakula mbalimbali na mimea vinavyoweza kuwa tiba nzuri na kinga ya magonjwa.

Post a Comment

0 Comments