Header Ads Widget

Responsive Advertisement

KUMBUKUMBU | MIAKA 19 BAADA YA AJALI YA MV BUKOBA

bk2

Pichani ni mnara wa kumbukumbu ya eneo ambalo walizikwa watu waliopoteza maisha katika ajali ya MV Bukoba hiyo mnamo Mei 21.1996.

Kila mwaka  ifikapo Mei  21, kama siku ya leo watanzania tunakumbuka  tukio la ajali mbaya iliyowahi kutokea katika nchi yetu ya kuzama kwa meli ya MV Bukoba ndani ya ziwa Victoria, mnamo mwaka 1996. Kwa hali hiyo watanzaia tunaendelea kuwaombea ndugu  na jamaa waliotangulia mbele za haki.

Mtandao wako bora wa habari wa #RoryaFinestBlog,  unaungana na watanzania wote popote walipo kwa pamoja kuwaombea mema waliotangulia mbele za haki katika ajali hiyo, mbaya kabisa nchini mwetu.
Pia mishumaa ya amani na upendo kwa ndugu na familia  tunaiwasha kwa pamoja siku hii ya leo na mwisho tunamalizia kwa kusema ‘AMEN’.
Ajali ya kuzama kwa Mv Bukoba ilitokea katika ziwa Victoria mnamo tarehe 21/5/1996 na kupoteza maisha ya zaidi yawatu 1000. Ambao baadhi yao walizikwa katika kaburi la pamoja.
mv-bukobaPicha ya kumbukumbu  iliyokuwa ikionekana wakati wa ajali hiyo ya MV Bukoba…

Post a Comment

0 Comments