Mbunge wa viti maalum CCM Juliana Shonza alipata nafasi ya kuchangia katika bajeti kuu ya serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017. Licha ya kuipongeza serikali katika jitihada zake lakini hajaridhishwa na tatizo la vifo vya wazazi vinavyoendelea kujitokeza nchini kwa kukosa huduma za kiafya ikiwemo zahanati.