Header Ads Widget

Responsive Advertisement

PLAY GIRL=6

Play gal – 06
Ilipoishia..
...Yule mlinzi akaushikilia ufunguo
wake wa getini vizuri huku
anamuita bosi wake Jerry kwa
sauti akienda mpaka mlangoni
nakutaka kuingia...
Endelea...
Yule mlinzi alifungua ule mlango nakuingia
mpaka ndani..
"..Aisha huyu mlinzi naona hatujui vizuri
enh.."
Nilimwambia Aisha huku kila mmoja
akipandisha nguo yake vizuri tayari kwa
nakuruka ukuta japo haukuwa mrefu sana..
Ndani ya muda mchache kila tulikuwa nje ya
geti huku tukifurahia kitendo tulichomfanyia
Jerry.
"..sasa shosti tukafanye shangwe wapi..?"
"..hilo tu wala usihofu, we twende pale
'nyumbani lounge' tukaburudike na mdada
Jide kisha turudi zetu hostel..
***
Ilituchukuwa mwendo wa kama nusu saa
kwa mwendo wa bajaj huku tukifurahia kwa
mbwembwe zote..
Ilipotimia mida ya saa 8 usiku Aisha alikuwa
kalewa sana ila kwa upande wangu nilikuwa
bado niko freshi, hivyo tukatoka nje nakukodi
tena bajaj mpaka chuoni kwetu Cbe zilipo
hostel.
Ndani ya dakika chache tayari tulikuwepo
hostel, nilimkokota Aisha wangu mpaka
bwenini, tukajipumzisha japokuwa akili
yangu ilikuwa haipo pale kabisa, kila muda
nilitamani japo nipige simu ya Jerry nijue
kama tumempa ulemavu wa maisha au
limekufa kabisa..
"..naombea nisikie limekufa hata sasa hivi.."
Nilijisemea kimoyo moyo huku nikiuweka
mto vizuri tayari kwa kulala..
Kesho yake asubuhi na mapema ambapo
Aisha alikuwa bado na uchovu kalala fofofo,
nilichukuwa simu yangu nakutuma meseji ya
kiuchokozi kwa Jerry huku nikiamini kwa
asilimia zote itajibiwa tu, niliandika hivi..
'..Mambo Jerry, miss u..!'
Kweli haikupita muda nikapigiwa simu..
"..hallow.."
"..sorry, naongea na Jerry..?"
Sauti niliosikia ni tofauti na ile ya Jerry..
"...Jerry yupo hapa Ocean road kalazwa yupo
hoi toka usiku wa leo kwani we nani
mwenzangu.."
Nikajichekea kimya kimya na kwa dharau
huku nikiendelea kumdadisi yule mtu..
"..jamani mpe pole sana sana, mchana wa leo
nitakuja kumuangalia, mie ni rafiki yake
naitwa Tina.."
Nilipomaliza tu kuongea na simu, nilishikwa
na furaha ya ajabu huku mwili ukinisisimka
nakuamini alichonifanyia mara ya mwisho
kwake tayari nimeshalipizia. .
Ilipofika mida ya saa 5 tano tano, Aisha naye
alikuwa ameshahamka hivyo nikamwelezea
kila kitu, nakumwambia yeye abaki mie
nitaenda huko hospital kuhakikisha..,
Kwakujifanya na mie nilikuwa nampenda
Jerry nikanunua Juici kubwa ya box na
matunda matunda mchanganyiko, kama
kawaida kichwani nikajifuka kwa mtandio
huku chini nikiwa na gauni refu lenye
heshima, nikiwa ndio nakaribia tu hospitali
ya 'Ocean road' nikanyanyua simu nakupigia
tena ile namba ya Jerry..
"..samahani, unaweza kunielekeza wodi
aliyolazwa..?"
"..njoo huku 'block C' wodi namba 4 single.."
Nilifuata maelekezo mpaka hapo, na
nilipoingia nilikutana na wasichana wengi
kama 10 na, huku wakiwa wameleta vyakula
mbalimbali, wanaume walikuwa wawili tu
huku baadhi ya wasichana wakishindwa
kujizuia nakulia kwa sauti ya juu..
Jerry bado alikuwa usingizini hivyo
nilishindwa kumuona akiongea..
Yule niliyekuwa naongea naye kupitia simu ya
Jerry ni ndugu yake kabisa na Jerry, nilipofika
yeye ndiye alikuwa karibu yangu sana
nakunipa maendeleo ya Jerry alivyoambiwa
na dokta..
Nikuwa itamchukuwa muda mrefu kupona
haswa lile eneo la juu ya nanii yake..
Matamanio mengine yakanianza hapo..
"..duh, Kumbe ndugu zake Jerry wazuri, dah
ila sidhani kama atakuwa na tabia kama za
Jerry.."
Niliusemea moyo huku nikimpa vile vitu
nilivyoleta. Kama kawaida Tina mie
nikishaonaga wanaume weupe tu akili yote
inahama nakuanza matamanio..
Nilijikaza Tina mie nakumuongelesha yule
mkaka..
"...samahani naweza kukwambia kitu, mie
nataka kuondoka.."
"..bila samahani wala usihofu.."
Alinifuata nikamtoa mpaka nje nakuanza
maongezi naye..
"..najua utashtuka kukuita huku lakini
nachoweza kukwambia ni kwamba..."
Kabla sijamalizia kuongea, yule kaka
akapigiwa simu akapokea, alivyomaliza tu
kuongea na simu akanyong'onyea ghafla..
"...Ohh my God..!! Jerry hatunaye tena...
Nikabaki na mshangao huku siamini amini,
tukajikuta wote tunakimbia mpaka wodini
kuhakikisha kama kweli Jerry kafa..
Tulipofika tu wodini wasichana walikuwa
bado wamemzunguka Jerry huku wakimlilia
zaidi,
"..itakuwa kafa kweli nini..?"
Niliusemea moyo huku nikijipenyeza katikati
ya wale wasichana.
Tabasamu kubwa alilokuwa analitoa ndicho
kitu kilichowatoa zaidi machozi wakinadada
waliokuwa wanamlilia, Jerry alikuwa hajafa
japokuwa alikuwa hawezi kuongea lakini
macho yake yaliweza kuangaza huku na kule..
Bado swali moja lilinisumbua kichwa, ninani
aliyemwambia ndugu yake Jerry kwenye simu
kama Jerry kafa..?
Nilimshika tena mkono kwa mara ya pili yule
ndugu yake na Jerry mpaka nje..
"..embu niambie vizuri nani aliyekwambia
Jerry amekufa..?"
"..anhaa, ile simu nilipigiwa na mjomba na
nikweli Jerry amefariki.."
"..Jerry..? Jerry gani sasa..?"
"..Huyo mjomba wetu naye anamtoto anaitwa
Jerry ujue jina la Jerry ni la marehemu babu
yetu, sasa huyo mtoto wake mjomba alizaliwa
akiwa na moyo mkubwa, na aliugua sana,
ndio hivyo tena kazi ya mungu haina
makosa.."
"..dah, poleni sana.."
Nilisisimka kana kwamba na mie ni ndugu
wao tena ukarimu niliomuoneshea huyu
kaka..
"..kwa hapa Dar unakaa wapi..?"
"..mh, nakaa kinondoni pale 'mkwajuni.."
Alinijibu huku akinionesha tabasamu
nakunifanya nisisimke tena huku nikiuangalia
'lips' zake mara mbili mbili jinsi zilivyokuwa
pana..
"..hata kama wanamatatizo, sijui wamefiwa,
sijui wanauguza, mie hilo wala silitambui,
huyu
Kaka kweli simuachi.."
Niliusemea moyo huku nikimrembulia macho
nakuvilazimisha vidimpozi vyangu feki..
"..ok, lakini unaonekana kama umeoa enh.."
"..we bado umri haujafika, ndio kwanza nipo
mwaka wa kwanza pale Ifm.."
"..sasa hapo kinondoni unaishi na nani..?"
"..pale nimeamua kupanga tu kachumba
kamoja, sipendi kukaa hostel.. Wewe unakaa
wapi..?"
Kabla sijamjibu dokta akaja maeneo yale
tulipokuwa naye nakuongozana naye mpaka
ofisini..
Nilirudi kumuangalia Jerry kinafiki kujua
anahali gani..
Kwa kipindi hiki alikuwa kafunga macho
kuonesha kuwa anausingizi sana, nilitamani
nichukuwe sindano pale pembeni yangu
nakumchoma tena nanilii yake..
Kitendo alichonifanyia Jerry cha kuniingilia
kinyume na maumbile ndicho kilichoniuma
sana nakumchukia Jerry kila nilipokuwa
namuangalia pale kitandani..
"..na kama amenipa ukimwi, naurudisha tena
kwenye ukoo wao, nitahakikisha natembea
na ndugu zake mpaka nawamaliza.."
Hasira kali nilizokuw nazo ilinibidi
kuzipunguza kwa kutoka nje kabisa huku
nikimsubiria John 'ndugu yake Jerry' atoke
huko ofisini kwa dokta..
Haikumchukuwa muda sana nikamuona John
ametoka huku akionekana mwenyehuzuni
sana..
"..enhe vipi dokta kakwambiaje..?"
Nilimuuliza kwa shauku ya hali ya juu..
"...Dah, 'bro' maendeleo yake yanatia huruma,
na nikija kumjua aliyemfanyia hivyo, atanijua
kama mimi natokea Pemba ama Unguja.."
"..ok, niambie basi kitu gani umeambiwa na
dokta..?"
"..ni kwamba bro Jerry anapata shida sana
kukojoa, hivyo watamfanyia upasuaji mdogo
ili kupata njia nyingine yakutolea mkojo. Na
vile vile kunamshipa ambao unatumika
kupitishia 'sperm' (manii/ shahawa) nao
ulichanjwa ukawa wazi hivyo anaweza
akakosa uwezo wa kuzalisha tena maishani
mwake.."
Pale pale nikajifanya kama muvi za kibongo
nikaanza kutoa machozi yakinafiki huku
nikilazimisha kukohoa na makamasi kuyavuta
yalioambatana na chafya bandia..
Alinibembeleza sana, lakini ni kama
alinizidishia sauti, kwani nilizidisha sauti kana
kwamba nimefiwa.
Umati wa wauguzi pamoja na wapita njia
ndio walionisaidia kuninyanyua pale chini
nilipokuwa natapatapa huku nikilitaja jina la
Jerry mara nyingi nyingi.
John alinibeba akisaidiana na wapita njia
mpaka kwenye gari ya Jerry kisha,
"..unaishi wapi nikupeleke..?"
Aliuliza John kwa hasira, kwani nilivyolia kwa
sauti kulimkera sana, kumbe mie nilikuwa na
mtego wangu.. Nikashusha pumzi huku
nikijifuta machozi feki nakumuangalia John..
"..nipeleke kwako kwanza
nikabadilishe nguo yangu ya ndani
imechafuka sana, niko katika mwezi.."
Nilimdanganya ili iwe rahisi kuwa naye lakini
alionesha kama kushtuka kitu,
"..lakini mbona hapa kuna vyoo na unaweza
kubadilisha tu.."
"..kama hutaki nishushe, kwani hapa kuna
mabafu? Nataka nioge kabisa.."
"..ok, mie niko tayari kukupeleka hadi kwako
hata kama ni mbali..
"..naishi hostel, na leo Jumapili wanaume
kibao bwenini.."
Hadi mwenyewe akakubali nakuliwasha gari
nakuelekea kwake, furaha ya ajabu
iliyoamsha mshawasha wangu huku
nikijiamini kwa asilimia zote huko tuendako
lazima anifanye tu..
Ile tunafika njia panda ya kuelekea kinondoni,
John akapigiwa simu lakini hakupokea
alichoniambia nipokee halafu niweke 'laudi
spika' kwakuwa yeye anendesha gari,
"..halow.."
"..vipi mpenzi wangu J uko wapi? Mi niko
kwako hapa..
=>nawaombeni kila anayesoma awe ana
share sana,ili nipost mara nyingi.
Itaendelea kesho saa tatu asubuh , usikosee, toa maoni
Photo: Play gal – 06
Ilipoishia..
...Yule mlinzi akaushikilia ufunguo
wake wa getini vizuri huku
anamuita bosi wake Jerry kwa
sauti akienda mpaka mlangoni
nakutaka kuingia...
Endelea...
Yule mlinzi alifungua ule mlango nakuingia
mpaka ndani..
"..Aisha huyu mlinzi naona hatujui vizuri
enh.."
Nilimwambia Aisha huku kila mmoja
akipandisha nguo yake vizuri tayari kwa
nakuruka ukuta japo haukuwa mrefu sana..
Ndani ya muda mchache kila tulikuwa nje ya
geti huku tukifurahia kitendo tulichomfanyia
Jerry.
"..sasa shosti tukafanye shangwe wapi..?"
"..hilo tu wala usihofu, we twende pale
'nyumbani lounge' tukaburudike na mdada
Jide kisha turudi zetu hostel..
***
Ilituchukuwa mwendo wa kama nusu saa
kwa mwendo wa bajaj huku tukifurahia kwa
mbwembwe zote..
Ilipotimia mida ya saa 8 usiku Aisha alikuwa
kalewa sana ila kwa upande wangu nilikuwa
bado niko freshi, hivyo tukatoka nje nakukodi
tena bajaj mpaka chuoni kwetu Cbe zilipo
hostel.
Ndani ya dakika chache tayari tulikuwepo
hostel, nilimkokota Aisha wangu mpaka
bwenini, tukajipumzisha japokuwa akili
yangu ilikuwa haipo pale kabisa, kila muda
nilitamani japo nipige simu ya Jerry nijue
kama tumempa ulemavu wa maisha au
limekufa kabisa..
"..naombea nisikie limekufa hata sasa hivi.."
Nilijisemea kimoyo moyo huku nikiuweka
mto vizuri tayari kwa kulala..
Kesho yake asubuhi na mapema ambapo
Aisha alikuwa bado na uchovu kalala fofofo,
nilichukuwa simu yangu nakutuma meseji ya
kiuchokozi kwa Jerry huku nikiamini kwa
asilimia zote itajibiwa tu, niliandika hivi..
'..Mambo Jerry, miss u..!'
Kweli haikupita muda nikapigiwa simu..
"..hallow.."
"..sorry, naongea na Jerry..?"
Sauti niliosikia ni tofauti na ile ya Jerry..
"...Jerry yupo hapa Ocean road kalazwa yupo
hoi toka usiku wa leo kwani we nani
mwenzangu.."
Nikajichekea kimya kimya na kwa dharau
huku nikiendelea kumdadisi yule mtu..
"..jamani mpe pole sana sana, mchana wa leo
nitakuja kumuangalia, mie ni rafiki yake
naitwa Tina.."
Nilipomaliza tu kuongea na simu, nilishikwa
na furaha ya ajabu huku mwili ukinisisimka
nakuamini alichonifanyia mara ya mwisho
kwake tayari nimeshalipizia. .
Ilipofika mida ya saa 5 tano tano, Aisha naye
alikuwa ameshahamka hivyo nikamwelezea
kila kitu, nakumwambia yeye abaki mie
nitaenda huko hospital kuhakikisha..,
Kwakujifanya na mie nilikuwa nampenda
Jerry nikanunua Juici kubwa ya box na
matunda matunda mchanganyiko, kama
kawaida kichwani nikajifuka kwa mtandio
huku chini nikiwa na gauni refu lenye
heshima, nikiwa ndio nakaribia tu hospitali
ya 'Ocean road' nikanyanyua simu nakupigia
tena ile namba ya Jerry..
"..samahani, unaweza kunielekeza wodi
aliyolazwa..?"
"..njoo huku 'block C' wodi namba 4 single.."
Nilifuata maelekezo mpaka hapo, na
nilipoingia nilikutana na wasichana wengi
kama 10 na, huku wakiwa wameleta vyakula
mbalimbali, wanaume walikuwa wawili tu
huku baadhi ya wasichana wakishindwa
kujizuia nakulia kwa sauti ya juu..
Jerry bado alikuwa usingizini hivyo
nilishindwa kumuona akiongea..
Yule niliyekuwa naongea naye kupitia simu ya
Jerry ni ndugu yake kabisa na Jerry, nilipofika
yeye ndiye alikuwa karibu yangu sana
nakunipa maendeleo ya Jerry alivyoambiwa
na dokta..
Nikuwa itamchukuwa muda mrefu kupona
haswa lile eneo la juu ya nanii yake..
Matamanio mengine yakanianza hapo..
"..duh, Kumbe ndugu zake Jerry wazuri, dah
ila sidhani kama atakuwa na tabia kama za
Jerry.."
Niliusemea moyo huku nikimpa vile vitu
nilivyoleta. Kama kawaida Tina mie
nikishaonaga wanaume weupe tu akili yote
inahama nakuanza matamanio..
Nilijikaza Tina mie nakumuongelesha yule
mkaka..
"...samahani naweza kukwambia kitu, mie
nataka kuondoka.."
"..bila samahani wala usihofu.."
Alinifuata nikamtoa mpaka nje nakuanza
maongezi naye..
"..najua utashtuka kukuita huku lakini
nachoweza kukwambia ni kwamba..."
Kabla sijamalizia kuongea, yule kaka
akapigiwa simu akapokea, alivyomaliza tu
kuongea na simu akanyong'onyea ghafla..
"...Ohh my God..!! Jerry hatunaye tena...
Nikabaki na mshangao huku siamini amini,
tukajikuta wote tunakimbia mpaka wodini
kuhakikisha kama kweli Jerry kafa..
Tulipofika tu wodini wasichana walikuwa
bado wamemzunguka Jerry huku wakimlilia
zaidi,
"..itakuwa kafa kweli nini..?"
Niliusemea moyo huku nikijipenyeza katikati
ya wale wasichana.
Tabasamu kubwa alilokuwa analitoa ndicho
kitu kilichowatoa zaidi machozi wakinadada
waliokuwa wanamlilia, Jerry alikuwa hajafa
japokuwa alikuwa hawezi kuongea lakini
macho yake yaliweza kuangaza huku na kule..
Bado swali moja lilinisumbua kichwa, ninani
aliyemwambia ndugu yake Jerry kwenye simu
kama Jerry kafa..?
Nilimshika tena mkono kwa mara ya pili yule
ndugu yake na Jerry mpaka nje..
"..embu niambie vizuri nani aliyekwambia
Jerry amekufa..?"
"..anhaa, ile simu nilipigiwa na mjomba na
nikweli Jerry amefariki.."
"..Jerry..? Jerry gani sasa..?"
"..Huyo mjomba wetu naye anamtoto anaitwa
Jerry ujue jina la Jerry ni la marehemu babu
yetu, sasa huyo mtoto wake mjomba alizaliwa
akiwa na moyo mkubwa, na aliugua sana,
ndio hivyo tena kazi ya mungu haina
makosa.."
"..dah, poleni sana.."
Nilisisimka kana kwamba na mie ni ndugu
wao tena ukarimu niliomuoneshea huyu
kaka..
"..kwa hapa Dar unakaa wapi..?"
"..mh, nakaa kinondoni pale 'mkwajuni.."
Alinijibu huku akinionesha tabasamu
nakunifanya nisisimke tena huku nikiuangalia
'lips' zake mara mbili mbili jinsi zilivyokuwa
pana..
"..hata kama wanamatatizo, sijui wamefiwa,
sijui wanauguza, mie hilo wala silitambui,
huyu
Kaka kweli simuachi.."
Niliusemea moyo huku nikimrembulia macho
nakuvilazimisha vidimpozi vyangu feki..
"..ok, lakini unaonekana kama umeoa enh.."
"..we bado umri haujafika, ndio kwanza nipo
mwaka wa kwanza pale Ifm.."
"..sasa hapo kinondoni unaishi na nani..?"
"..pale nimeamua kupanga tu kachumba
kamoja, sipendi kukaa hostel.. Wewe unakaa
wapi..?"
Kabla sijamjibu dokta akaja maeneo yale
tulipokuwa naye nakuongozana naye mpaka
ofisini..
Nilirudi kumuangalia Jerry kinafiki kujua
anahali gani..
Kwa kipindi hiki alikuwa kafunga macho
kuonesha kuwa anausingizi sana, nilitamani
nichukuwe sindano pale pembeni yangu
nakumchoma tena nanilii yake..
Kitendo alichonifanyia Jerry cha kuniingilia
kinyume na maumbile ndicho kilichoniuma
sana nakumchukia Jerry kila nilipokuwa
namuangalia pale kitandani..
"..na kama amenipa ukimwi, naurudisha tena
kwenye ukoo wao, nitahakikisha natembea
na ndugu zake mpaka nawamaliza.."
Hasira kali nilizokuw nazo ilinibidi
kuzipunguza kwa kutoka nje kabisa huku
nikimsubiria John 'ndugu yake Jerry' atoke
huko ofisini kwa dokta..
Haikumchukuwa muda sana nikamuona John
ametoka huku akionekana mwenyehuzuni
sana..
"..enhe vipi dokta kakwambiaje..?"
Nilimuuliza kwa shauku ya hali ya juu..
"...Dah, 'bro' maendeleo yake yanatia huruma,
na nikija kumjua aliyemfanyia hivyo, atanijua
kama mimi natokea Pemba ama Unguja.."
"..ok, niambie basi kitu gani umeambiwa na
dokta..?"
"..ni kwamba bro Jerry anapata shida sana
kukojoa, hivyo watamfanyia upasuaji mdogo
ili kupata njia nyingine yakutolea mkojo. Na
vile vile kunamshipa ambao unatumika
kupitishia 'sperm' (manii/ shahawa) nao
ulichanjwa ukawa wazi hivyo anaweza
akakosa uwezo wa kuzalisha tena maishani
mwake.."
Pale pale nikajifanya kama muvi za kibongo
nikaanza kutoa machozi yakinafiki huku
nikilazimisha kukohoa na makamasi kuyavuta
yalioambatana na chafya bandia..
Alinibembeleza sana, lakini ni kama
alinizidishia sauti, kwani nilizidisha sauti kana
kwamba nimefiwa.
Umati wa wauguzi pamoja na wapita njia
ndio walionisaidia kuninyanyua pale chini
nilipokuwa natapatapa huku nikilitaja jina la
Jerry mara nyingi nyingi.
John alinibeba akisaidiana na wapita njia
mpaka kwenye gari ya Jerry kisha,
"..unaishi wapi nikupeleke..?"
Aliuliza John kwa hasira, kwani nilivyolia kwa
sauti kulimkera sana, kumbe mie nilikuwa na
mtego wangu.. Nikashusha pumzi huku
nikijifuta machozi feki nakumuangalia John..
"..nipeleke kwako kwanza
nikabadilishe nguo yangu ya ndani
imechafuka sana, niko katika mwezi.."
Nilimdanganya ili iwe rahisi kuwa naye lakini
alionesha kama kushtuka kitu,
"..lakini mbona hapa kuna vyoo na unaweza
kubadilisha tu.."
"..kama hutaki nishushe, kwani hapa kuna
mabafu? Nataka nioge kabisa.."
"..ok, mie niko tayari kukupeleka hadi kwako
hata kama ni mbali..
"..naishi hostel, na leo Jumapili wanaume
kibao bwenini.."
Hadi mwenyewe akakubali nakuliwasha gari
nakuelekea kwake, furaha ya ajabu
iliyoamsha mshawasha wangu huku
nikijiamini kwa asilimia zote huko tuendako
lazima anifanye tu..
Ile tunafika njia panda ya kuelekea kinondoni,
John akapigiwa simu lakini hakupokea
alichoniambia nipokee halafu niweke 'laudi
spika' kwakuwa yeye anendesha gari,
"..halow.."
"..vipi mpenzi wangu J uko wapi? Mi niko
kwako hapa..
=>nawaombeni kila anayesoma awe ana
share sana,ili nipost mara nyingi.
Itaendelea kesho saa tatu asubuh , usikosee, toa maoni

Post a Comment

0 Comments